Robo Mwezi. Massimo Longo E Maria Grazia Gullo

Чтение книги онлайн.

Читать онлайн книгу Robo Mwezi - Massimo Longo E Maria Grazia Gullo страница 3

Robo Mwezi - Massimo Longo E Maria Grazia Gullo

Скачать книгу

kazi. Hatimaye, akapata kazi katika mji tofauti. Kila siku alilazimika kusafiri muda mrefu na kubadilisha njia ya usafiri mara kadhaa, na kusababisha kuwa mbali na familia yake kwa saa nyingi kila siku. Hurejea nyumbani akiwa amechoka na akili yake kusubaa. Baada ya chakula cha jioni, analala kwenye kochi na bila shaka kuzama kwenye usingizi licha ya jaribio ya kutaka kuwa macho.

      Carlo alidokeza kuwa Elio anapaswa kutoa vipokea sauti vya maskioni. Elio alikubaliana naye tu ili kuepuka kukemewa.

      "Ni wakati wa chakula cha jioni. Njoo ule." Aliamuru. "Mamake alisema kuwa umekaa hapa tangu saa kumi jioni!"

      Elio aliamka kutoka kitandani, na huku akiangalia chini alitembea kupita mbele ya babaye. Na kisha akatembea kuelekea jikoni, bila hata kujaribu kujadiliana na babaye.

      Gaia tayari alikuwa ameketi mezani ambayo alikuwa ameandaa na alikuwa akiwatumia ujumbe rafiki zake na kufanya mipango nao.

      Elio aliketi mbele ya dadaye. Walakini hakuongea neno hata moja naye wakati wote wa chakula cha jioni.

      Chakula cha jioni kilibainika kuwa kisicho cha furaha. Kila mtu alikuwa akiongea kuhusu matukio yao ya kila siku, isipokuwa Elio, ambaye alikula vipande vichache vya nyama na kurejea kwenye chumba chake haraka iwezekanavyo. Mamaye alisikitishwa na ishara hiyo, na babaye pia ambaye alionekana kukunja uso.

      Wakati Giulia na Carlo waliachwa chumbani wakati walikuwa wanaondoa sahani mezani, walianza kuzungumzia mada iyo hiyo ya awali: tabia mbaya za mwanao.

      "Ni nini tunafanya vibaya? Hata siwezi kuelewa! Gaia ni mtu tendaji, mwenye furaha na mwenye hiba!" alisema Giulia

      "Nilimpuuza sana!" Carlo alijilaumu kama kawaida.

      "Wewe si baba pekee duniani ambaye analazimika kuwa mbali na nyumbani kwa saa nyingi. Mimi, kwa upande mwingine, niko nyumbani kila alasiri" Alirudia tena kwa kuwa hakutaka mumewe kuhisi kuwa na mzigo begani.

      "Sio swala la tabia, Giulia, kwa sababu Elio hakuwa hivi awali, na unaijua!"

      "Natamani pia kwamba asingekuwa hivi, Carlo, lakini watoto hubadilika wanapokua. Na kisha, wanazidi na kuzidi kuwa wabaya zaidi, sivyo? Akiwa shuleni ni balaa. Natarajia kuwa hatapinga, lasivyo hatutaweza kumpeleka kwenda kambi ya majira yajayo ya joto...hatutaweza kumruhusu kwenda shule wakati wa kiangazi...hatafurahia!"

      "Giulia, watoto wengine kwa kawaida huburudika shuleni wakati wa kiangazi. Watoto wa Francesca na Giuseppe wanafurahia sana. Unafahamu vyema kuwa hatafanya chochote kwenye kambi ya majira ya joto! Tunahitaji kutafuta chaguo jingine, kitu ambacho kitamfanya apambane. Hata haonekani kuwa na furaha. Je! Unakumbuka jinsi tulivyokuwa na nguvu wakati tulipokuwa na umri sawa na yake?"

      "Bila shaka, naikumbuka!" Mamangu angefoka kwenye mlango wetu kwamba chakula cha jioni kimekuwa tayari. Lakini, mara nyingi, hata singemsikia kwa kuwa nilikuwa na shughuli nyingi kwenye bustani nikijibingirisha kwenye nyasi. Tulikuwa na furaha na huru. Kwa kweli hatuwezi kumpa maisha kama hii mjini. Walakani, hajui jinsi ya kufurahia kambi ya majira ya kiangazi. Hana rafiki, hakuna tunayeweza kumwalika na kumsaidi kuponya tabia hii ambayo anaishi. Haruhusu mtu yeyote kushikamana naye. Wakati mwingine najiuliza jinsi anavyohisi kuhusu sisi. Anakwepa ninapojaribu kumkumbatia..."

      "Giulia, vijana hawataki kukumbatiwa na mama zao. Nina uhakika bado anatupenda, lakini hatuwasiliani naye kwa njia mwafaka. Tunahitaji kutafuta njia mpya. Tunahitaji kutafuta njia ya kumuamsha. Labda, angezungumza na Ida? Ana wavulana wawili wadogo. Labda anaweza akatupatia ushauri mzuri. "

      "Unaogopa anaweza geuka kuwa kama Libero? Kwamba anaugua ugonjwa unaorithiwa wa kisaikolojia?"

      "Hapana, kwa Libero ilikuwa tofauti. Matatizo yake yalitokana na kifo cha babaye. Lakini matukio hayo yanafanana na jinsi Ida anavyofahamu huenda ukafaa. Alifanya miujiza na kijana huyo baada ya kuhamia kijijini. Na alifanya yote hayo pekee yake! na shamba ilisaidia pia."

      "Ndio, umjulishe hayo. Naamini dadako. Ana njia yake ya kuangalia mambo, na ninapenda."

      "Tutaipata ripoti ya shule lini?" Carlo akamwuliza bibiye.

      "Juni 19..."

      "Tutakuwa tumechelewa kuamua kitu cha kufanya. Unapaswa kuuliza mwalimu wake wa Italia kuwa na mazungumzo ya moja kwa moja na wewe. Lazima tuamue ni wapi tunapeleka watoto wetu. Maombi ya kujiunga na kambi ya majira ya kiangazi na shule ya majira ya kiangazi yatafungwa kabla ya tarehe 19." alipendekeza Carlo.

      "Ndio, umesema ukweli. Tunahitaji kuwa na uhakika wa hali hiyo, ingawa hafanyi vibaya shuleni. Ni vile tu haweki royo yake katika chochote anachokifanya. Unafahamu kwamba wapangaji wapya wameingia orofa ya pili? Waonekana kuwa watu wazuri. Bi Giovanna aliniambia walihamia hapa kutoka Potenza. Hiyo ni mbali! Hakika haitakuwa raisi kwao mwanzoni. Wana mwana aliye na umri sawa na Elio. Nitamwalika aje mchana fulani..."

      Giulia kisha akagundua kuwa Carlo, ambaye alikuwa amelala kwenye kochi, tayari alikuwa amezama usingizini.

      "Njoo, mpenzi, twende tukalale kitandani." Alimnongoneza kwa upole ili amwamshe.

       Sura ya pili

       Mnong'ono wa baridi ulikuwa ukimsumbua

      Elio alikuwa amesimama kwenye njia pana ya miguu mbele ya shule yake. Watoto wengine wote waliokuwa karibu naye walikuwa wakiongeza kasi, wanaposhuka katika gari za wazazi wao au wakifukuzana wakiwa njiani kwenda nyumbani. Yeye kwa upande mwingine alikuwa akiangalia kila mahali kwa wasiwasi kwa gari ya mama yake kana kwamba ndio njia yake ya kuishi, akitarajia kwamba hajaondoka baada ya kukutana binafsi na mwalimu wake wa Italia.

      Baada ya kila mtu kuondoka katika yadi ya shule kwa muda mfupi, Elio aliacha kusubiri na kuanza kutembea kwenda nyumbani. Alichukia kutembea. Na alichukia hata zaidi kutembea chini barabara hiyo isiyovumilika iliyo na mstari wa miti ya ndimu inayounganisha shule na nyumba yao.

      Alisubiri dakika chache zaidi na kisha akaamua kuelekea nyumbani pekee yake. Kisha, akamuru mguu wake kusonga mbele. Kwa mtu mwengine yule inaweza kuonekana kama kazi raisi, lakini kwa Elio, ambaye mawasiliano yake na miguu yake ilikuwa haba, ilikuwa mapambano.

      Akageuka kushoto kupitia del Corso; akiwa kwa kona alijipata mbele ya barabara iliyonyooka ambayo aliidharau. Kijisitu cha miti ya ndimu ilipandwa kando kando ya barabara hiyo kuu. Kwa mtu mwengine yule ilikuwa tu kijisitu kizuri cha miti ya ndimu iliyochanua ambayo manukato yake yalibebwa na upepo, na kulifanya eneo hilo kunukia viruzi. Alipoanza kwenda chini kufuata mistari ya miti kwa ugumu, alihisi kuwa anafuatwa.

      Aligeuka kwa haraka na kufikiria kuwa alikuwa ameona mnyama mweusi amejificha nyuma ya mti.

      "Haiwezi kuwa" aliendelea kujirudia mwenyewe. "Je! Nimeona miwani katika pua la mbwa huyo wa ajabu?"

      Kwa hofu akaendelea kutembea, huku akiona vivuli nyuma ya miti. Isitoshe, upepo ulikuwa ukivuma kupitia matawi. Mnongono wa upepo ulikuwa unamhangaisha; ilikuwa ikikuna maskio yake na kisha kukwama kwenye akili yake.

      Hakuweza kuelewa maana ya sauti hizo. Huku akiwa ameshikwa na hisia hiyo mbaya, aliamuru mwili wake kujaribu na kukimbia. Alikuwa akitokwa na jasho, na akikimbia zaidi, sauti hizo zilizidi kuonekana kama zinamkimbiza na vivuli vikaonekana kuzidi kumkaribia.

      Alianza kukimbia kwa kasi na kwa uwezo wake wote. Kisha, alisikia sauti ya kikatili ikimwamuru kuacha kukimbia. Aligeuka mara moja na kwa mara nyingine aliona kitu ya sura nyeusi ikijificha nyuma ya mti uliokaribu. Alikuwa tayari amefika makutano na barabara kuu, ambayo ingeashiria mwisho wa ndoto hiyo.

      Hata

Скачать книгу