Robo Mwezi. Massimo Longo E Maria Grazia Gullo

Чтение книги онлайн.

Читать онлайн книгу Robo Mwezi - Massimo Longo E Maria Grazia Gullo страница 4

Robo Mwezi - Massimo Longo E Maria Grazia Gullo

Скачать книгу

hivyo, alihisi upepo baridi nyuma ya shingo yake. Aligeuka tena, mara hii bila kukimbia, lakini kitu kilimgonga vikali na kumtupa chini.

      Elio alishtuka na kujikunja kama mpira huku kichwa chake kikiwa kwenye mikononi mwake.

      Wakati uo huo, alisikia sauti anayoijua ikimwita:

      "Elio! Elio! Je! Unafanya nini?"

      Ilikuwa dada yake ambaye alikuwa akimkaripia. Alikuwa amekasirika kwa kuwa alikuwa amemkimbilia. Baadaye alitambua kuwa Elio alikuwa katika hali mbaya.

      Alitulia na kuuliza:

      "Unajisikiaje?"

      Elio, baada ya kusikia sauti yake, akainua kichwa chake.

      Gaia aligunduwa kuwa alikuwa amechanganyikiwa, anatoa jasho na uso wake ulikwajuka kuliko kawaida. Kwa sekunde, alijaribu kufikiria ni kwanini alikuwa akikimbia. Haikuwa kawaida kwake. Ilionekana kwake kwamba alikuwa akitoroka kitu au mtu. Wakati uo huo, alimsaidia kuinuka.

      "Kwanini ulikuwa ukikimbia hivyo?" alimwuliza. "Kuna kitu kilikutisha?"

      Gaia hakukumbuka mara ya mwisho Elio alikimbia. Elio hakujibu. Kitu pekee alichokitaka ni kuondoka barabarani haraka iwezekanavyo. Alipiga kona barabarani bila kusema lolote.

      Gaia akamfuata akiwa na wasi wasi.

      "Elio!" alimwita tena.

      "Hakuna kitu!" akajibu Elio kwa ujeuri. "Kwa kweli hakuna kitu!"

      Tabia ya Elio ilimfanya Gaia kukasirika tena.

      "Hakuna kitu, eeh? Ulinikimbia sawasawa. Na bado, unasema hakuna kitu!"

      Elio alimwomba msamahaili kuepuka majadiliano zaidi, only to avoid further discussions, ambayo ingechosha mwili wake hata zaidi.

      "Samahani." alisema.

      Misamaha hiyo ya juu juu iliishia kumkasirisha Gaia hata zaidi. Hata hivyo, aliendelea kutembea nyuma ya kakaye, huku akiwa na wasiwasi kumhusu.

      Kufikia Jumapili asubuhi, Carlo na Giulia hatimaye walikuwa wamefanya uamuzi. Wakati walipokuwa wanatengeneza kiamsha kinywa, walikuwa wakiongea kuhusu wazo hilo wakati wakisubiri watoto kuamka

      "Alikuwa mkarimu kutoa wazo kama hilo. Nataraji, hao watato watakuwa na tabia njema." alisema Giulia akiwa na tabasamu kubwa usoni.

      Ilikuwa uamuzi ngumu kufanya, lakini Carlo na yeye walikuwa wanahisi shauku ya ajabu kuihusu, kwa vile walikuwa wamekubaliana nayo.

      "Gaia atafurahi." alisema Carlo. "Elio, kwa upande mwingine, atasalia kutojali kama kawaida."

      "Sina uhakika...Gaia alifanya urafiki na watoto wengine katika kambi ya majira ya joto. Atakasirika. Na kuhusu Elio, atachukia hata hivyo." akasema Giulia.

      "Siwezi kusubiri tena. Nitawaamsha." akapendekeza Carlo kwa uthabiti, na kutembea kwenda vyumba vyao akiwaita kwa majina yao.

      Hakuniruhusu hata kusafisha uso wao.

      "Mama yako na mimi tuliamua kile utakachofanya wakati wa majira ya joto. Shule itafungwa Ijumaa na Jumapili Asubuhi mtapelekwa kwa kituo cha reli!"

      "Lakini kambi ya majira ya joto haitaanza kwa majuma mengine mawili yajayo!" Gaia alisema kwa wasi wasi na kumtazama mama yake. Kutoka mlango wa jikoni, alikuwa akitazama kile kilichokuwa kikiendelea kwenye ushoroba.

      "Kwa kweli, hutaenda kwenye kambi ya majira ya joto mwaka huu" akajibu Giulia na kwa kufanya hivyo, alithibitisha hofu ya Gaia. "Tulifikiri tutakupa fursa ya kutumia wakati wako wa majira ya joto kwa mtindo wa zamani; jinsi tulivyofanya wakati tulipokuwa na umri kama yako. "

      "Hiyo inatakikana kumaanisha nini?" akauliza Gaia, wakati Elio alikuwa kimya na mwenye sura mbaya.

      "Utakuwa nje, kimbia hadi upungukiwe na pumzi, ogelea kwenye bwawa na utumie usiku wa majira ya joto kwenye maonesho mtaani" akajibu Carlo kwa bintiye.

      Gaia aliweza kuona wazazi wake wakiangaliana na kucheka, na kwa haraka akafikiria walikuwa wakiwafanyia mzaha.

      "Acha kutufanyia mzaha. Mnashida gani asubuhi hii?"

      "Hiyo si mzaha. Shangazi Ida amejitolea kuwakaribisha wakati wa majira ya joto." Hatimaye Carlo akafichua kwa watoto wake, ambao walikuwa wakimwangalia bila kuamini.

      "Hii ni ndoto mbaya. Ninarudi kulala!" akasema Gaia, ambaye alionekana kukasirika.

      "Nilifikiria utafurahi " akasema babaye.

      "Kufurahi? Tayari nilikuwa nimewasiliana na rafiki zangu! Nimesubiri wakati wote wa msimu wa baridi!"

      "Gaia, utapata rafiki kwa shangazi pia." Mtie moyo Giulia.

      "Lakini kwanini nitake kufanya hivo? Ninapenda kuwa na rafiki katika kambi ya majira ya joto. Ninaweza kukaa nje na kupiga mbizi ziwani. Sitaki kuwa mahali pengine."

      "Ndio, hutaki. lakini Elio anataka. Anahitaji kubadilisha hewar." Akaongeza Carlo.

      "Nilijua!" akaropoka. "Ni kwa sababu ya Elio! Na mbona asiende kwa shangazi Ida pekee yake?"

      "Hatutaki aende pekee yake." akasisitiza Giulia.

      "Mimi si yaya wake!"

      "Lakini wewe ni dada yake mkubwa. Mbona husemi kitu, Elio?" akauliza Carlo.

      Elio hakusema lolote. Akainua mabega yake, na kuathiri akili ya Gaia.

      "Hivyo? Hakuna? Hakuna swala muhimu wkako. Haya! ambia mama na baba kwamba hutafanya chochote shambani pia."

      Elio aliinama na kukubaliana naye.

      "Acha, Gaia! Acha kufanya hivi! Tayari tumeshaamua. Binamu yako Libero atakuchukua kituoni" tamatisha mazungumzo Carlo.

      Gaia akakimbia, akionekana kufa moyo na kukasirika.

      "Atakuwa sawa." akasema Giulia, akijua starehe ya maisha ya bintiye.

      Elio alirudi kwenye chumba chake bila kutambuliwa.

      Carlo alishangaa. Hata hivyo, alikuwa na uhakika kwamba uamuzi wao ulikuwa bora katika kwa miaka mingi.

      Ijumaa ilifika haraka. Carlo alimchukua mpwa wake kutoka kituoni na kufurahi alipofikiria kumkumbatia tena.

      Libero alikuwa na furaha, mvumilivu na mvulana asiye wa kawaida. Alikuwa mrefu na mwembaba, lakini mifupa yake haikudhihirikamwilini. Uso wake ulikuwa umepigwa na jua, mikono yake ilikuwa kubwa na alikuwa akifanya kazi katika shamba la familia yake. Macho yake ya kijani yalionekana wazi kwenye ngozi yake, na nywele zake fupi za kahawia zilikuwa zimegawanyika kama mtu aliye na umri wa miaka 50. Alimkumbatia mjomba wake kwa nguzu na tangu wakati huo hakuacha kuongea.

      Carlo alikuwa akimwangalia akishangaa. Alikumbuka vizuri wakati Libero alikuwa mgonjwa, asiyejali na mwenye kukasirika haraka. Ingawa Libero hakuwa mwerevu sana, lakini maisha raisi aliyokuwa akiishi yalimfurahisha. Na Carlo alikuwa akitaka Elio akubali chanya ya binamu yake. Wakati uo huo, Libero alikuwa akisukuma pua lake kwenye dirisha la gari na alikuwa anauliza swali kuhusu kila kitu aliona njiani.

      Kila

Скачать книгу