Robo Mwezi. Massimo Longo E Maria Grazia Gullo

Чтение книги онлайн.

Читать онлайн книгу Robo Mwezi - Massimo Longo E Maria Grazia Gullo страница 5

Robo Mwezi - Massimo Longo E Maria Grazia Gullo

Скачать книгу

mtu nyumbani alikuwa akimsubiri.

      Giulia alikuwa na wasiwasi wakati alipokuwa akifunga vitu vya mwisho. Wakati umefika na alikuwa akijiuliza iwapo mambo yatakuwa mazuri. Licha ya hayo, yeye alikuwa mama yao na hakuweza kujizuia ila kuwa na wasi wasi.

      Gaia, kwa upande mwingine, alikuwa amekubaliana na wazo hilo. Alikuwa anamkimbiza mama yake ndani ya nyumba akiwa na maelfu ya maswali: aliweza kuona nini? Angefanya nini shambani?

      Elio nay eye hawakuwa wameenda shambani tangu walipokuwa watoto wakati wazazi wa baba yao walikuwa hai. Hawakuwa na kumbukumbu yoyote ya mahali hapo, isipokuwa kumbukumbu: mashamba, au manukato ya miti iliyo nyuma ambayo iliwasadia kucheza mchezo wa kujificha na kutafuta.

      Baada ya mumewe kuaga dunia, shangazi Ida alijitahidi kurudisha maisha yake. Basi, aliamua hamia kwa wazazi wake pamoja na watoto wake na kutelekeza shamba lake la zamani.

      Mara tu aliposikia sauti za funguo zikifungua kufuli, Gaia alikimbia kuelekea kwa binamu yake, ambaye alimwinua na kumzungusha kama ilivyo kwenye jukwaa la kujiburudisha. Gaia alitabasamu kwa kuwa hakutarajia maonesho kama hayo ya mapenzi.

      "Habari, Libero. Umekuaje?" alimwuliza kwa uchangamfu binamu yake ambaye alikuwa hajaonana naye kwa muda mrefu.

      "Vizuri, mpenzi." akajibu Libero.

      Wakati uo huo, Giulia alijiunga nao na Libero alimsalimia kama muungwana, akimpa busu ya haraka mara mbili kwmashavu yote mawili.

      "Safari ilikuwa aje?" akauliza Giulia.

      “Vizuri sana, "ngombe huyo wa chuma" ina kasi sana na ina raha wakati unataka kusafiri; na jiji limejaa vitu vya kupendeza kuona. Ninafuraji kuwa hapa!"

      "Tafadhali keti. Lazima umechoka. Je! Ungependa aiskrimu?" akauliza Giulia.

      "Ndio, asante, Shangazi." Nimepokea kwa furaha Libero. "Wapi Elio?"

      "Elio yuko katika chumba chake. Atakuwa hapa baada ya dakika chache." rakajibu Carlo. Alikuwa amekasirika kwa sababu mwanawe hakujisumbua hata kuja kusalimia binamu yake, ambaye amesafiri mwendo mrefu ili kumchukua. Alipoanza kutembea kuelekea kwenye chumba cha Elio,

      Libero alianza kuongea:"Usijali, mjomba Carlo. Nitaenda. Nataka kumshangaza. Niambie tu chumba chake ni kipi."

      Mara tu Carlo alipomwonesha chmba cha Elio, Libero akamka kuelekea mlangoni. Kilio cha furaha cha Libero kilisikika kwenye ushoroba wakati alipokuwa akimsalimia binamu yake.

      Hata Elio, licha ya utulivu wake hakuweza kuepuka kukumbatiwa na Libero.

      Gaia alimtazama mamaye na kunong'ona:

      "Sikukumbuka kwamba alikuwa anaweza kudanganywa hivyo!"

      "Usiseme hivyo." Maramoja akamkaripia Giulia. "Ni mvulana mzuri. Na ni mwema sana pia."

      "Ndio, lakini... Unauhakika atatuendesha salama hadi tufike shambani." Bila shaka aliuzila Gaia.

      "Kweli, hiyo atafanya!" akamtuliza Carlo. "Usimdharau. Yeye na mama yake anaendeleza kazi ya shambani. Yeye ana nguvu na ni mwerevu."

      Wakati wa chakula cha jioni ulifika na kuendelea kwa furaha. Kwa kweli, Libero alikuwa amemletea sherehe zote na uchangamfu wa vijijini, ambayo ilithaminiwa san ana kila mtu isipokuwa Elio.

      "Nasubiri sana kukuonesha huku." Alimaliza Libero baada ya kueleza mambo ya shamba kwa binamu yake.

      "Una uhakika kwamba hutaki kukaa kwa siku kadhaa kabla ya kuondoka tena?" akauliza Giulia.

      "Siwezi kumwacha mama pekee yake wakati huu wa mwaka. Kuna mambo mengi ya kufanya."

      "Uko sahihi, Libero. Kwa kweli wewe ni mvulana mzuri." akamsifu Carlo, akimpapasa kwa upole begani.

      "Unajua, mjomba Carlo, nilikuwa najiuliza kitu. Kabla ya kuja huku mjini, nilifikiria unatakiwa kupiga honi tu wakati wa dharura...."

      "Ndio, hiyo ni kweli." akajibu Carlo. "Kwanini?"

      "Kwa sababu inaonekana kila mtu hutumia kana kwamba walikuwa wanacheza muziki kwenye sherehe! Hawaachi kupiga honi!"

      Kila mtu aliangua kichezo, isipokuwa Elio, ambaye alijiuliza iwapo Libero alikuwa akitania au la ...

       Sura ya tatu

       Aligundua kuwa mvulana huyo alikuwa ametishika, na akaangua kicheko

      Asubuhi ya siku iliyofuata Libero alimtoa Giulia kwenye kitanda chake baada ya kujikwa kwenye zulia la ushoroba. Kwa hivyo, Giulia na yeye walijikuta wakila kiamsha kinywa kabla ya kila mtu kuamka. Wakati harufu ya kahawa safi ilipokuwa iliovamia chumba cha kulala cha Carlo, pia alielekea jikoni na kuanza kuelezea kile kilichokuwa kimemekabili Elio siku za hivi karibuni.

      "Usijali." aliwahakikishia Libero. "Uzoefu huu wa nje utamsaidia. Na mama tayari ana mkakati! "

      Mara tu walipofika kituo cha gari moshi, Giulia hakuweza kuacha kutoa mapendekezo na kuhakikisha kuwa watoto watakuwa na tabia nzuri.

      Gaia hakuweza kusubiri; alikuwa amesisimika na mdadisi. Kwa upande mwingine, ilikuwa wazi kwamba Elio alikuwa akiburuzwa tu kwenye hayo. Zaidi ya hayo, pia alikuwa amebeba mizigo mizito ya Gaia kwa sababu tu Libero alimfanya kufanya hivyo: "Wanawake hawapaswi kubeba uzito!" alisema, ambayo ilisababisha Elio atumbue macho. Hakuweza kumvumilia binamu yake tayari.

      Libero alikuwa amevaa suruali ya khaki, t-shati na kofia ya kujikinga ya baseball ya manjano, ambayo ilionekana isiyofaa kabisa kwa binamu zake. Zaidi ya hayo, alikuwa amebeba mizigo iliyobaki kwa wepesi kiasi kwamba inaweza ilikuwa haina kitu ndani.

      Treni iliondoka kwa wakati ufaao. Hakuna mtu mwengine aliyekuwa ndani ya gari walilokuwa wametengewa. Baada ya Libero kupanga mizigo yote kwenye juu ya gari, alipendekeza:

      "Gaia, andamana nami. Hebu tuende kwenye mgahawa wa gari na tupate kiamsha kinywa zaidi. Itakuwa safari ndefu na utahitaji nguvu zako zote. Elio anaweza kuchunga mizigo. Hata hakuna mtu atakayeikaribia. Ikiwa mtu atagusa, bweka! " alisema Libero kwa binamu yake. "Na ukiacha kukasirika, tunaweza hata kukuletea chakula..."

      Gaia na Libero walitoka nje ya gari, na kumpa Elio faraja kubwa kwa kuwa alitaka kuwa peke yake.

      Alikuwa akiangalia mandhari ya nje kupitia dirisha lake. Walikuwa wamesafiri kupita eneo la viwanda la jiji na walikuwa wameanza kuzungukwa na mashamba na milima ambayo ilikuwa ikibadilishana tena na tena.

      Ghafla, kwenye kidirisha cha dirisha akaona sura ya mzee amekaa kwenye kiti cha kando kiti chake.

      Aliingia lini kwenye gari? Hakusikia milango ikifunguliwa.

      Mzee huyo alikuwa amevaa nguo nyeusi na alikuwa amevaa miwani isiyo ya kawaida puani. Alikuwa akisoma kitabu cheusi cha ngozi ambacho kilionekana kama cha karne moja kilichopita, ambacho kurasa zake zilitengenezwa kwa karatasi ya tishu. Kichwani alikuwa na kofia yenye kuta pana iliyokuwa inaficha uso wake. Mandhari yote ilikuwa isiyo ya kutuliza.

      Elio hakugeuka, lakini alikuwa akimwangalia kupitia akisi kwenye kidirisha cha dirisha. Alihisi kuogopa kuwa peke yake na mtu huyo. Wakati huo kwa hakika alitaka binamu yake mkubwa na mwenye nguvu awe karibu naye. Walakini, yeye wala Gaia hawakuwa wakionekana.

      Wakati uuo huo,

Скачать книгу